Showing posts with label kimataifa. Show all posts
Showing posts with label kimataifa. Show all posts

Wednesday, 2 November 2016

Serikali ya DRC yatakiwa kuimarisha usalama katika mji wa Bunia


Na Neema  Dandida
 
 












Harakati ya Vijana wa Bunia katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imewataka viongozi wa serikali kuchukua hatua za lazima kwa ajili ya kuimarisha usalama katika mji huo wa kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.

Harakati hiyo ya vijana wa mji wa Bunia ambao ni makao makuu ya mkoa wa Ituri ulioko kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imebainisha katika taarifa yake kwamba, maafisa wa setrikali katika mji huo wanapasawa kuchukua hatua za lazima kwa ajili ya kuimarisha usalama wa raia na mali zao katika mji huo.

Harakati hiyo imesisitiza kwamba, kumetokea mashambulio ya silaha katika siku za hivi karibuni katika maeneo tofauti ya Bunia pamoja na viunga vya mji huo. Silvain Agernowoth, Mratibu wa Harakati ya Vijana wa Bunia amewaambia waandishi wa habari kwamba, raia wa mji huo siku ya Jumamosi na Jumapili za wiki iliyopita walifanikiwa kuzima hujuma na mashambulio saba pasina ya uingiliaji wa polisi.
 












Uwanja wa ndege wa Bunia 

Raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wanaamini kuwa, kutokuwa na uwezo jeshi la nchi hiyo na askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataigfa nchini humo MONUSCO wa kuyatokomeza makundi ya waasi ni jambo ambalo limechangia kwa sehemu kubwa kuenea ukosefu wa usalama na amani katika maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo.

Eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo limekuwa likishuhudia machafuko kwa zaidi ya miaka 20 sasa kutokana na kuwa ngome ya makundi kadhaa ya waasi kutoka nchi jirani za Rwanda na Uganda.

Baadhi ya vijiji vya mashariki mwa nchi hiyo vinadhibitiwa na makundi ya waasi hali ambayo imewafanya wakazi wake kuyaacha makazi yao na kuwa wakimbizi.
Chanzo pars today

Uzalishaji mafuta warejea katika hali yake ya kawaida nchini Nigeria

Na Neema Dandida
Waziri wa Mafuta wa Nigeria amesema kuwa, uzalishaji mafuta umerejea katika hali yake ya kwaida nchini humo.

Shirika la habari la IRIB limemnukuu Emmanuel Ibe Kachikwu akisema hayo jana na kuongeza kuwa, uzalishaji mafuta nchini Nigeria umefikia mapipa milioni mbili na laki moja kwa siku jambo ambalo linaonesha kufikiwa kiwango chake cha kawaida cha kabla ya kuharibiwa taasisi za kuzalisha mafuta za nchi hiyo.

Wiki chache zilizopita, serikali ya Nigeria ilifanya mazungumzo na kundi la waasi wa Niger Delta la kusini mashariki mwa nchi hiyo kwa upatanishi wa mashirika ya kigeni na jeshi la polisi kwa lengo la kulitafutia ufumbuzi tatizo la ukosefu wa amani ambalo limeathibiri vibaya eneo hilo kwa muda mrefu sasa.

Uharibifu wa mabomba ya mafuta mara nyingi hufanyika kwa lengo la kuiba mafuta hayo, na jambo hilo limekuwa la kawaida sana nchini Nigeria, ambayo ni mzalishaji mkuu wa mafuta ghafi barani Afrika.

Waziri wa Mafuta wa Nigeria amesema, mazungumzo baina ya serikali na waasi yamekuwa na mafanikio makubwa. Amesema, malengo ya mwaka 2017 ya nchi yake ni kumaliza kabisa vitendo vya uharibifu vinavyofanywa na makundi mbalimbali ya nchi hiyo.
Sehemu kubwa ya mafuta ghafi ya Nigeria yanazalishwa katika eneo la Niger Delta la kusini mashariki mwa nchi hiyo. 

Asilimia 80 ya bajeti ya Nigeria inategemea uuzaji nje mafuta ghafi ya nchi hiyo.
                             chanzo pars today

Uzalishaji mafuta warejea katika hali yake ya kawaida nchini Nigeria

Na Neema Dandida
Waziri wa Mafuta wa Nigeria amesema kuwa, uzalishaji mafuta umerejea katika hali yake ya kwaida nchini humo.

Shirika la habari la IRIB limemnukuu Emmanuel Ibe Kachikwu akisema hayo jana na kuongeza kuwa, uzalishaji mafuta nchini Nigeria umefikia mapipa milioni mbili na laki moja kwa siku jambo ambalo linaonesha kufikiwa kiwango chake cha kawaida cha kabla ya kuharibiwa taasisi za kuzalisha mafuta za nchi hiyo.

Wiki chache zilizopita, serikali ya Nigeria ilifanya mazungumzo na kundi la waasi wa Niger Delta la kusini mashariki mwa nchi hiyo kwa upatanishi wa mashirika ya kigeni na jeshi la polisi kwa lengo la kulitafutia ufumbuzi tatizo la ukosefu wa amani ambalo limeathibiri vibaya eneo hilo kwa muda mrefu sasa.

Uharibifu wa mabomba ya mafuta mara nyingi hufanyika kwa lengo la kuiba mafuta hayo, na jambo hilo limekuwa la kawaida sana nchini Nigeria, ambayo ni mzalishaji mkuu wa mafuta ghafi barani Afrika.

Waziri wa Mafuta wa Nigeria amesema, mazungumzo baina ya serikali na waasi yamekuwa na mafanikio makubwa. Amesema, malengo ya mwaka 2017 ya nchi yake ni kumaliza kabisa vitendo vya uharibifu vinavyofanywa na makundi mbalimbali ya nchi hiyo.
Sehemu kubwa ya mafuta ghafi ya Nigeria yanazalishwa katika eneo la Niger Delta la kusini mashariki mwa nchi hiyo. 

Asilimia 80 ya bajeti ya Nigeria inategemea uuzaji nje mafuta ghafi ya nchi hiyo.
                             chanzo pars today

Rais Mugabe Aidhinisha 'sarafu mpya' Zimbabwe

 Na Neema Dandida
 
Rais Robert Gabriel Mugabe wa Zimbabwe

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ametumia mamlaka ya ofisi yake kutoa dikrii inayoidhinisha matumizi ya sarafu mpya nchini humo, licha ya asasi za kiraia kusisitiza kuwa uamuzi huo ni kinyume cha sheria.
Patrick Chinamasa, Waziri wa Fedha wa Zimbabwe amesema Mugabe ametumia kifungu cha 133 cha Sheria ya Mamlaka ya Rais ya 2016, kuidhinisha matumizi ya sarafu hiyo inayoshabihiana na Dola ya Marekani na kufafanua kuwa, kwa sasa ni halali kutumia sarafu hiyo katika mabadilishano ya bidhaa na huduma mbalimbali.
  
Patrick Chinamasa, Waziri wa Fedha wa Zimbabwe.
Hata hivyo aliyekuwa Waziri wa Fedha wa nchi hiyo, Tendai Biti, amekosoa uamuzi huo wa Mugabe na kusema kuwa ni wa kidikteta na unaokiuka katiba ya nchi.

Nchi ya Zimbabwe imekuwa ikikabiliwa na changamoto za kifedha hasa baada ya kushuka thamani ya sarafu yake kuanzia mwaka 2009 na kuamua kuanza kutumia Dola ya Marekani.
Tangu kipindi hicho, mbali na Dola ya Marekani, raia wa Zimbabwe wamekuwa wakitumia sarafu zingine za kigeni kama Yuro, Yuan ya China, Pauni ya Uingereza na Rand ya Afrika Kusini.

  Maandamano dhidi ya serikali nchini Zimbabwe.

Katika siku za hivi karibuni, Zimbabwe imekuwa ikishuhudia maandamano ya wapinzani wanaomtaka Rais Mugabe mwenye umri wa miaka 92 aondoke madarakani wakisisitiza kuwa ameshindwa kutatua matatizo ya kiuchumi na ukosefu wa ajira nchini humo.
                                 Chanzo Pars Taday

Rouhani: Uingiliaji wa kigeni umeleta mgawanyiko Mashariki ya Kati


 Na Neema Dandida
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema matatizo yanayolikabili eneo hili la Mashariki ya Kati yamesababishwa na uingiliaji unaofanywa na nchi za kigeni katika masuala ya ndani ya nchi za eneo hilo.
Katika mazungumzo yake na Demetris Syllouris, Rais wa Bunge la Cyprus hapo jana mjini Tehran, Rais Rouhani alisema, ili kuwa na mustakbali wenye mwangaza, maendeleo, usalama na ututivu, nchi za eneo hili sharti zishirikiane na kila moja itekeleze wajibu wake wa kimataifa.
Rais Hassan Rouhani ameelezea kusikitishwa kwake na namna mamilioni ya watu wasio na hatia katika nchi za Iraq, Syria, Yemen na Libya wanavyoendelea kukabiliwa na matatizo chungunzima kutokana na migawanyiko, uhasama na mapigano yaliyochochewa na nchi za Magharibi.


Mazungumzo ya Rais Hassan Rouhani na Demetris Syllouris, Rais wa Bunge la Cyprus Tehran
Kwengineko katika mazungumzo hayo, Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza umuhimu wa kuimarishwa uhusiano kati ya Tehran na Nicosia na kubainisha kuwa, ushirikiano huo unaweza kuwa daraja ya kuunganisha Mashariki ya Kati na bara Ulaya pamoja na bara Afrika.
Kwa upande wake, Demetris Syllouris, Rais wa Bunge la Cyprus amesema kuchukuliwa hatua za kijeshi katika kuitafutia ufumbuzi migogoro inayolikabili eneo la Mashariki ya Kati, hakujakuwa na natija nyingine ghairi ya kuzidisha mizozo hiyo na kuibua mingine mipya. Amesema kuwa Cyprus iko tayari kuimarisha uhusiano wa pande mbili na Iran katika nyuga za biashara, uchumi na utamaduni.
Rais wa Bunge la Cyprus ambaye aliwasili nchini Jumapili iliyopita kufuatia mwaliko wa Spika wa Majilisi ya Ushauri ya Kiislamu, Ali Larijani, amekutana na kufanya mazungumzo na maafisa mbalimbali wa ngazi za juu wa serikali ya Tehran akiwemo Mohammad Javad Zarif, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran
Chanzo Pars Today

Sunday, 12 June 2016

Rais Obama alaani mauaji ya Orlando



Rais wa Marekani,Barack Obama amelaani mauaji yaliyotokea Orlando













Rais wa Marekani,Barack Obama amesema shambulio la risasi katika Klabu ya usiku mjini Orlando ni la kigaidi na ni kitendo cha chuki

Takriban watu 50 wamepoteza maisha na wengine 53 wamejeruhiwa siku ya Jumapili, baada ya mtu mmoja aliyekuwa na silaha kufyatulia risasi Klabu moja ya usiku iliyokuwa ikiwakutanisha watu wa mapenzi ya jinsia moja mjini Orlando nchini Marekani.

Polisi nchini humo wamesema kuwa ni shambulio baya halikuwahi kutokea katika historia ya nchi hiyo.

Rais Obama amesema Marekani inaungana ikiwa na huzuni,mshtuko mkubwa na inalenga kutetea watu wake, pia amesema mauaji hayo yanawakumbusha ni namna gani ilivyo rahisi kupata silaha hatari nchini Marekani.

Shirika la kijasusi nchini humo,FBI limemtambua mshambuliaji huyo kuwa raia wa Marekani,Omar Mateen ambaye naye aliuawa wakati wa mapambano na vikosi vya usalama katika klabu hiyo ambayo ilikuwa na zaidi ya watu 300 ndani yake.

              chanzo bbc swahili